Dar es Salaam--Inakadiriwa pia kuwa ifikapo mwaka 2020 magojwa ya
kuambukiza yatakuwa na uwiano sawa na magonjwa yasiyoambukiza. Hii inatokana na
magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama maradhi ya moyo kuongezeka miaka hadi miaka.
Moja ya mambo ambayo yamekuwa yakichangia kuongezeka kwa
matatizo ya moyo ni ulaji wa chumvi. Chumvi ni moja ya kiungo kinachoweka ladha
katika vyakula.
''Chumvi ni muhimu pia mwilini. Huusaidia mfumo wa fahamu katika kutekeleza kazi zake, kujivuta kwa misuli, udhibiti wa kiwango sahihi cha maji na uwiano sahihi wa chumchumvi mwilini''
Chumvi hutumika pia kwa ajili ya kudhibiti wingi wa maji
katika damu, ogani na tishu za mwilini. Pale chumvi inapozidi basi figo huwa na
kazi ya kuitoa kwa njia ya mkojo.
Chumvi ikiwa nyingi figo hushindwa kutoa kiasi chote na
kubakia mwilini hivyo kusababisha matatizo.
Watu wengi hula chumvi nyingi na hujikuta wakiongeza
wanapopatiwa chakula. Wengi hawafahamu kama ulaji chumvi kwa mtindo huu ni
hatari kwa afya zao.
Msukumo wa damu mwilini hutegemea na uwepo chumvi na pale
inapozidi mwilini msukumo wa damu nao unakuwa juu. Hali huwa mbaya kwa yule
ambaye tayari ana matatizo ya moyo. Watu ambao kwao kuna historia ya shinikizo
la damu ni vizuri kuchunga na kupunguza matumizi ya chumvi katika chakula.
Chumvi nyingi husababisha magonjwa mengine kama vile
kiaharusi. Hii hutokea pale msukumo wa damu unapokuwa mkubwa zaidi na
kusababisha mishipa ya damu kuathirika.
Mishipa ya artery huweza kuharibika na kuwa myembamba au
kusinyaa na kuta zake hukukaamaa. Hali hii huufanya moyo kuwa na kazi ngumu na
hivyo inakuweka katika hatari ya kupata shambulizi la moyo la ghafla, moyo
kushindwa kufanya kazi au kiharusi.
Matatizo mengine ni kama vile moyo kuwa mkubwa na valvu kuwa
na matatizo. Hii inatokana na ujazo mkubwa katika mzunguko wa damu, hivyo
kuufanya moyo uwe na kazi ya ziada ili kuwa na mzunguko sahihi unaotakiwa na
mwili.
Kadiri muda unavyosonga na uwepo wa hali hii husababisha
moyo kuongezeka ukubwa na valvu za moyo huwa nyembamba. Hali hii husababishamaumivu
ya kifua, kushindwa kupumua na kuwa na uchovu usioisha. Pia kifo cha ghafla na
moyo kushindwa kufanya kazi huweza kutokea.
Chumvi pia husababisha magonjwa mengine kama ya figo, mwili
kuvimba na upungufu wa maji, tindi kali kuwa nyingi tumboni na udhaifu wa
mifupa.
Namna ya kutumia chumi ipo kanuni ya dole gumba. Kiasi
unachofinya ndicho kinatakiwa kiwepo kwenye kila mlo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni